WAZIRI Mkuu wa Somalia Abdi Farah Shirdon ameapa “kuwafuta” al-Shabaab
waliotekeleza shambulizi kwenye jengo moja la kibiashara nchini Kenya.
"Tuna zaidi ya askari 17,000 wa AMISOM (askari wa
Umoja wa Afrika) nchini Somalia na kwa kusaidiana na wananchi wetu na jumuiya
ya kimataifa, nina imani tutawamaliza al-Shabab," anasema bwana Shirdon.
Anasema kuwa nchi yake kwa kushirikiana na Kenya
wataendelea kupambana na wapiganaji hao kwa kuwa ni tatizo linalozisibu nchi
hizo kwa pamoja na kwamba Mogadishu haitakubaliana na matakwa ya al-Shabaab ya
kutaka vikosi vya Kenya viondoke Somalia:
“Tatizo la Al-Shabab
sio tatizo la Somalia peke yake, ni tatizo ya ukanda mzima, na jumuiya ya
kimataifa kwa ujumla…tunapambana na adui yetu sote.
"Hatuna tatizo na ndugu zetu wa Kenya…Wapo Somalia
kwa ombi la Somalia, wapo kama sehemu ya jeshi la AMISOM na tunashirikiana
katika kupambana na al-Shabaab,” alisema.
Aliongeza kusema kuwa, “Nina furaha kwamba tutawadhibiti
na hivi karibuni hawatatusumbua tena, inshaallah.”
Mapema Jumamosi, wapiganaji wa al-Shabab walifanya
shambulio kwenye jengo la kibiashara la Westgate mjini Nairobi, ambalo hatimaye
lilikombolewa mapema Jumanne.
Kwa uchache raia 61 na wanajeshi 6 waliuawa katika
shambulizi hilo. Idadi ya mwisho ya vifo bado haijatangazwa.
Kundi la al-Shabab lilidai kuhusika na shambulio hilo,
likisema kuwa walifanya hivyo kujibu mapigo ya uwepo wa askari wa Kenya nchini
Somalia.
0 comments:
Post a Comment