AL-SHABAAB: TULIUA WATU 137 WESTGATE

 



NAIROBI, KENYA: Wakenya na ulimwengu mzima wanasubiri kwa shauku kjua idadi kamili ya vifo vya shambulizi la Westgate baada ya washambuliaji kudai kuwa waliua watu 137.

Familia zilipoteza watu wao wametishika sana huku wataalamu wa kuchunguza mauaji wakichelewa kutoa miili ya wale waliokutwa na mauti katika jengo hilo.

Mashirika ya habari ya BBC na Associated Press yaliandika katika akaunti zao za twitter kwamba Al-Shabaab waliripoti kwamba waliwaua watu 137.

Vikosi vya usalama viliripoti kuwa sauti za mateka zilisikika wakati wa dakika za mwisho za harakati za vikosi vya pamoja kulidhibiti jengo hilo baada ya sehemu ya jengo hilo kuanguka.

Askari sita wa jeshi la Kenya ni miongoni mwa watu 69 waliouawa, kwa mujibu wa rekodi rasmi zilizotolewa na mamlaka za serikali. Askari hao walihusika katika juhudi za kuwaokoa mateka waliokuwa wameshikiliwa na watekaji.

Inaamini kuwa idadi ya mwisho itajulikana baada ya wataalamu hao kuruhusu utoaji wa miili iliyofukiwa na kifusi ndani ya jengo hilo.  Mashuhuda waliofanikiwa kukimbilia eneo salama walisema kuwa waliona miili kadhaa ya maiti ikiwa imelala sakafuni.


CHANZO: KTN Kenya
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment