RAIS YAHYA JAMMEH: USHOGA NA USAGAJI NDIO KITISHO KIKUBWA ZAIDI DUNIANI





Katika hotuba yake jana mbele ya Hadhara kuu ya Umoja wa Mataifa, Rais wa Gambia, Yahya Jammeh, aliwashambulia mashoga na wasagaji na kusema kuwa vitendo hivyo ni miongoni mwa “vitisho vikubwa kabisa kwa uwepo na uhai wa jamii ya binadamu.”

Rais Jammeh alisema kuwa ushoga, tamaa na ubabe “ni majanga makubwa kabisa kuliko majanga yote ya kiasili yakiwekwa pamoja.”

Maneno haya ya Rais Jammeh ni muendelezo wa msimamo wake dhidi ya vitendo vya ushoga na usagaji. Mwaka 2008, aliwaambia mashoga na wasagaji kuondoka nchini mwake la sivyo wakatwe vichwa.

Vilevile amekuwa akiandamwa na ukosoaji wa kimataifa kwa kusema kuwa anaweza kutibu UKIMWI kwa dawa yake ya asili na ya mitishamba.


Rais Yahya Jammeh aliingia madarakani katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi mwaka 1994 kwa njia ya mapinduzi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment