PICHA MAALUMU ZA KISIWA KILICHOIBUKA BAADA YA TETEMEKO LA ARDHI HUKO PAKISTAN




Umbali wa mita kadhaa kutoka ufukwe wa Pakistan limetokea jambo la ajabu jana Jumanne tarehe 24 Septemba baada ya tetemeko kubwa la ardhi lililoupiga mji wa Aoran katika jimbo la Balochistan lililo kusini magharibi mwa Pakistan na kuua watu wasiopungua 328.

Ghafla kilionekana kisiwa mkabala na mji wa Gawadar kusini magharibi mwa nchi hiyo. Kisiwa hicho kina takriban urefu wa mita 200, upana ni mita 100 huku urefu wa kwenda juu ukiwa ni mita 20. Hayo ni kwa mujibu wa Dk Asef Inam kutoka chuo cha taifa cha sayansi za bahari.





Lakini suala hilo limeibua swali: Je, kisiwa hicho kimetokana na tetemeko hilo? Wataalamu wanatilia shaka suala hilo wakisisitiza kuwa “tetemeko lilitokea mbali na mji wa Gawadar na kwamba matetemeko kama hayo hayawezi kuleta matokeo ya aina hiyo.”  Kwa mujibu wa mtafiti kutoka Chuo Kikuu cha Oregon Chris Gould Wenger, tetemeko la Tsunami ndilo linaloweza kusababisha matokeo kama hayo ya kutokezea kwa kisiwa.

Hivyo basi, suala hilo linabaki kuwa lenye utata. Isipokuwa baadhi ya waandishi wa habari wanadai kuwa kisiwa husika kiliibuka miaka 45 iliyopita kikapotea mwaka mmoja baada ya kuibukuka kwake.

CHANZO: France 24/ Arabic


PICHA MBALIMBALI ZA KISIWA HICHO





















Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment