MAAFA MAKUBWA PAKISTAN

 A family of Pakistani earthquake survivors sit with their belongings near their collapsed mud houses in the Mashkail area of southwest Baluchistan Province.


MAAFISA wa Pakistan wanasema kuwa kwa uchache watu 327 wamethibitika kupoteza maisha na mamia kujeruhiwa baada ya tetemeko thakili la ardhi kulipiga jimbo la kusini magharibi la Balochistan.

Zaidi ya watu 400 wamejeruhiwa katika tetemeko hilo lenye ukubwa wa 7.8 lililoitikisa miji kadhaa kama vile Karachi, Hyderabad, Quetta na Kalat.

Ripoti za vyombo vya habari kutoka nchini humo zinasema kuwa mifumo ya mawasiliano imeharibiwa vibaya sana katika maeneo hayo.

Maafisa wa hali ya hewa wanasema kuwa mitikisiko ilisikika mpaka kwenye miji mingine kama mji mkuu wa India, New Delhi. Mitetemo mingine midogo ilifuatia na kuutikisa ukanda wote wa eneo hilo.


Jeshi la Pakistan limelazimika kuingia kazini kufanya shughuli za uokozi na kuwasambaza askari wapatao 200 katika eneo lote.


Jimbo la Balochistan ni eneo linalokumbwa na matetemeko ya mara kwa mara. Tetemeko kama hilo liliua watu 41 mwezi Aprili. 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment