Naibu Waziri wa Elimu nchini Sierra Leone, Mamoud Tarawali
ameshitakiwa kwa makosa ya kumbaka mwanafunzi wa chuo kikuu, polisi walisema.
"Anakabiliwa na mashitaka ya kubaka, kujeruhi,
kushambulia na kudhuru kwa kukusudia. Amenyimwa dhamana na sasa yupo katika
jela ya Pademba,” mkuu wa polisi Francis Munu, alisema siku ya Jumanne.
Wiki iliyopita, Tarawali alifikishwa kwa pilato kwa
tuhuma za ubakaji. Siku ya Jumatatu alikuwa mahakamani kusikiliza mashitaka
yakisomwa na aliyanusha yote.
Polisi wanasema kuwa mashitaka hayo yaliwasilishwa na
mwanafunzi mwenye umri wa miaka 24 kutoka chuo kikuu cha Sierra Leone cha mjini
Freetown aliyesema kuwa alibakwa na Tarawali katika eneo la faragha.
Sierra Leone inajaribu kuponya majeraha ya vita vya muda
mrefu, ambapo wapiganaji walifanya kila aina ya dhulma za kingono dhidi ya
wanawake na mabinti na matukio hayo yakashamiri.
- Reuters
0 comments:
Post a Comment