DAR WAFURAHIA KUONDOLEWA POLISI JAMII

 


BAADHI ya wakazi wa jijini Dar es Salaam wamefurahia kuondolewa kwa kikosi cha Polisi Jamii ambacho kiligeuka kuwa kero.

Wakizungumza kwa wakati tofauti jijini Dar es Salaam jana, wananchi wengi walisema serikali ilikurupuka katika uamuzi wake wa kuunda kikosi hicho bila maandalizi ya msingi.

Wakiomba majina yao yahifadhiwe, wananchi hao walisema kuwa hatua ya serikali ya kukiondoa kikosi hicho inadhihirisha namna walivyokosea tangu awali, ingawa kulikuwa na nia njema.

“Hebu fikiria hao polisi jamii walikuwa ni wezi, vibaka, watuamiaji wakubwa wa dawa za kulevya na walevi wa pombe haramu ya gongo ambao hawakupewa mafunzo yaliyostahili. Badala yake walikuwa wala rushwa wakubwa na mamlaka yao yalizidi yale ya Jeshi la Polisi,” alisema mmoja  wa wakazi wa Gongo la Mboto jijini Dar es Salaam.

“Sijui walitumia vigezo gani kuwapata  hao waliojiita Polisi Jamii, maana utakuta mtu ambaye alikuwa mbabe wa mtaa ndiye amepewa hiyo nafasi, jambo ambalo si sahihi na hilo liliwafanya wajifanyie kazi kiholela pasipo maadili, maana walikuwa ovyo ovyo tu,” aliongeza mkazi huyo.

Hata hivyo, alikiri kuwa ingawa baadhi ya sehemu walitoa msaada mkubwa lakini kwa sehemu kubwa hawakusaidia chochote na ndiyo maana uhalifu haukwisha, kwani vibaka na wezi wote ni marafiki zao.

Kikosi cha Polisi Jamii kiliondolewa hivi karibuni kutokana na baadhi ya madereva na wakazi mbalimbali ya Jiji la Dar es Salaam kulalamikia utendaji kazi wao ambao ulikuwa ukipita mipaka ya Jeshi la Polisi.


CHANZO: Tanzania Daima
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment