MTOTO WA JENERALI HUKO CHINA AHUKUMIWA ADHABU YA KIFUNGO KWA UBAKAJI

 


MAHAKAMA moja nchini China imemhukumu mtoto wa jenerali mmoja wa nchi hiyo kifungo cha miaka 10 jela kwa kosa la kubaka, baada ya kesi yake kuvuta hisia za wananchi.

Li Tianyi, mwenye umri wa miaka 17, na wanaume wengine wanne wamekutwa na hatia ya kumbaka mwanamke mmoja katika hoteli moja mjini Beijing mwezi Februari mwaka huu.

Baba yake anaitwa Li Shuangjiang, ni mwimbaji katika jeshi na ana cheo cha jenerali katika jeshi la China.


Wakati wa kesi yake, vyombo vya habari viliripoti kuwa “hakukiri kufanya hujuma ya kingono na hakukiri kuwa na uhusiano na mwanake husika, akisema kuwa alikuwa amelewa na hakujua chochote” kilichotokea.

Washtakiwa wengine wanne katika kesi hiyo walihukumiwa adhabu ya kifungo cha kati ya miaka 3 na 12.

Baadhi ya watu walikuwa na wasiwasi kwamba Li asingehukumiwa adhabu ya kifungo gerezani. Wengine walifurahishwa na hukumu hiyo iliyotolewa jana alhamisi.

Baba yake ni mkuu wa idara ya sanaa katika chuo cha jeshi la China, na ni maarufu kwa nyimbo za kizalendo. Mama yake, Meng Ge, naye pi ni mwimbaji mkubwa.


CHANZO: Al-Jazeera
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment