Licha ya Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya kutangaza ushindi
dhidi ya watekaji wa jengo la kibiashara la Westgate mjini Nairobi, wapiganaji
wa al-shabaab wamesisitiza kuwa wataendelea kupambana.
Akizungumza na kituo cha televisheni cha Aljazeera,
msemaji wa operesheni za kijeshi wa kundi hilo, Sheikh Abdulaziz Abu Muscab, alimtaka
Rais Kenyatta kuyaondoa majeshi yake nchini Somalia, la sivyo mashambulizi
mengine ya kigaidi yapo njiani.
Muscab alieleza kuwa Kenya ndio adui yao mkubwa katika
ukanda huu na kuonya kuwa shambulizi la Westgate si lolote mbele ya
yatakayotokea iwapo Kenya haitaondoka Somalia.
“Kenya ni adui yetu wa kihistoria. Kenya ni adui wa watu
wa Somalia na nchi ya Somalia. Hatuamini kama Kenya ni jirani mwema. Hatuwaamini
na tutawapiga sana kwa sababu ni adui zetu”, alisema Muscab.
0 comments:
Post a Comment