Mwanamke anayedaiwa kuongoza kundi la wavamizi lililovamia
jengo la kibiashara la Westgate, Samantha Lewthwaite inadhaniwa kuwa ameuawa.
Lewthwaite, ambaye anaitwa kwa jina la utani la ‘Mjane
Mweupe’ anadaiwa kuongoza shambulizi hilo lililosababisha vifo vya watu 62 na
kujeruhi wengine 170 mjini Nairobi.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Mail la Uingereza,
mwanamke huyo inasemekana aliuawa juzi usiku na wanajeshi wa Kenya
wanaoshirikiana na maofisa wa Shirika la Ujasusi la Israel (Mossad) na wale wa
Shirika la Upelelezi la Marekani (FBI).
Hata hivyo, viongozi wa usalama wa Kenya hawakutaka
kuingia kwa undani juu ya taarifa za kifo cha Lewthwaite.
Kwa muda mrefu, Lewthwaite amekuwa akiwakimbia polisi
kwa kuvaa hijab akitembelea kati ya nchi za Tanzania, Somalia na Kenya.
Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari, mwanamke
huyo amekuwa akiishi kwa kujificha na amefanikiwa kutumia pasi za kusafiria za
nchi tofauti.
Amekuwa akitambulika kama raia wa Uingereza na Australia
lakini inasemekana amekuwa pia akitumia pasi ya kusafiria inayoonyesha kwamba
yeye ni raia wa Afrika Kusini akitumia jina bandia la Natalie Faye.
0 comments:
Post a Comment