KITUO CHA POLISI CHASHAMBULIWA MPAKANI MWA KENYA NA SOMALIA


Kenyan soldiers take cover after heavy gunfire near Westgate mall in Nairobi on September 23, 2013.
Askari wa Kenya wakijiandaa kukabiliana na wavamizi katika kituo cha biashara cha Westgate, Nairobi, tarehe 23/9/2013


MAAFISA wawili wa Polisi nchini Kenya wameuawa katika shambulizi lililotekelezwa dhidi ya kituo kimoja cha polisi katika mji wa kasikazini wa Mandera, mpakani mwa Somalia.

Kamanda wa polisi katika eneo hilo, Charlton Mureithi, anasema kuwa watu watatu pia walijeruhiwa katika shambulizi hilo lililotokea leo asubuhi, huku magari kumi yakiteketea kwa moto.

Mashuhuda wanasema kuwa watu wenye silaha walikishambulia kituo hicho kwa mabomu ya kurushwa kwa mkono kisha wakakimbia na kukiacha kituo hicho kikiwaka moto.

“Hakuna aliyekamatwa mpaka sasa. Wamesababisha uharibifu mkubwa,” alisema Mureithi.

Hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulizi hilo, ambalo limetokea siku moja baada ya raia mmoja kuuawa na wengine wanne kujeruhiwa katika shambulizi kama hilo katika mji wa kaskazini mashariki wa Wajir.

Mashambulizi hayo yametokea siku chache baada ya kundi la al-Shabab kukivamia kituo kimoja cha biashara mjini Nairobi na kuua watu 70 huku sehemu ya jengo hilo ikiharibiwa vibaya sana.

Jana Jumatano, kiongozi wa al-Shabaab, Ahmed Godane, alithibitisha kuwa kundi lake lilihusika na shambulizi la Nairobi, kwa madai kuwa walifanya hivyo katika kulipa kisasi cha uvamizi wa jeshi la Kenya kusini mwa Somalia mwezi Oktoba 2011.

“Ondoeni majeshi yenu, la sivyo jiandaeni kwa vita ya muda mrefu, umwagaji damu, uharibifu na kuwahamisha kwa nguvu,”  alisema Godane katika ujumbe wa sauti uliowekwa kwenye tovuti moja inayohusishwa na al-Shabab.

Kenya ina zaidi ya askari 4,000 kusini mwa Somalia, ambapo imekuwa ikipambana na al-Shabaab tangu mwaka 2011.


Askari wa Kenya ni sehemu ya Kikosi cha Umoja wa Afrika kwa ajili ya Somalia (AMISOM).
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment