YOGA HUPUNGUZA HATARI YA VYANZO VYA MARADHI YA MOYO



Utafiti mpya umeeleza kuwa mazoezi ya ‘yoga’ yanaweza kuwasaidia watu kupungumza hatari ya vyanzo vya maradhi ya moyo, hususan kama hawawezi kufanya aina nyingine ya mazoezi yanayotumia nguvu.

Utafiti huo mpya uliochapishwa jana katika Jarida la European Journal of Preventive Cardiology ulibaini kuwa yoga ina faida na manufaa muhimu, ikiwemo kushusha kiwango cha hatari ya unene wa kupindukia, shinikizo la damu na kolesteroli iliyozidi.

Watafiti hao walikuwa wamechambua tafiti 37 za mwanzo zilizowahusisha watu wapatao 3,000 nchini Uholanzi.

Mtafiti Myriam Hunink, kutoka kituo cha Afya cha Chuo Kikuu cha Erasmus mjini Rotterdam, anasema kuwa “Yoga ina faida za kupunguza vyanzo vya hatari sawa na faida zinazopatikana katika mazoezi ya kukimbia au kuendesha baiskeli.”

Maureen Talbot, muuguzi mwandamizi katika Taasisi ya Moyo ya Uingereza anasema kuwa faida za Yoga “zinaweza kuwa zinatokana na ufanyaji kazi wa misuli na kupumua, ambapo inaweza kuingiza hewa nyingi ya ‘oxygen’ mwilini, jambo linaloweza kupunguza shinikizo la damu.”


Yoga ni aina ya mazoezi ya kale yenye asili ya India takribani miaka 5,000 iliyopita. Mazoezi hayo hujumuisha mikao maalumu ya mwili, mazoezi ya kupumua, mbinu za kupumzika na kutafakari, na inahusishwa na faida nyingine nyingi za kiafya.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment