
Siku Moja baada ya kujiuzuri kwa Mwanasheria mkuu Jaji
Fredrick Werema, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna
Tibaijuka kwa mara nyingine amejitokeza hadharani na kutoa msimamo wake kwamba
hana sababu ya kujiuzuru kwenye nafasi yake kwa kuwa hakuhusika kwa namna
yeyote kwenye sakata la uchotwaji wa mabilioni kwenye akaunti ya Escrow.
Akizungumza na waandishi wa habari asubuhi jijini Dar es
Salaam, Profesa Tibaijuka amesema kuwa pamoja na kuwepo kwa shinikizo la kutaka
kujiuzuru, yeye binafsi ameona hana sababu ya kufanya hivyo kwani kufanya hivyo
ni kukubali kuwa amehusika moja kwa moja kwenye kashfa hiyo jambo ambalo si la
kweli.
Profesa Tibaijuka amekwenda mbali zaidi na kusema kuwa
uvumi unaoendelea kusambazwa mitaani ni ishara mbaya kwani unawaaminisha
wananchi kuwa amehusika katika sakata hilo wakati yeye hajahusika na jambo
lolote.
“Huu uvumi unatakiwa kuachwa, sioni sababu yeyote ya
mimi kujiuzuru kwa kuwa sijahusika kwa
namna yeyote kwenye sakata hili la Escrow” anasema Profesa Anna Tibaijuka.
TIBAIJUKA: Nikijiuzulu hata Rais atanishangaa maana
katika yale mapendekezo ya Bunge hakuna sehemu iliyonitaka kujiuzulu.
TIBAIJUKA: Niliomba mchango wa Shule nikapewa na
Rugemalira, sasa kujiuzulu nitakuwa sijaitendea haki jamii
TIBAIJUKA: Lengo la kuzungumza na Waandishi wa habari ni
kuzungumza yale niliyokosa nafasi ya kujitetea wakati wa sakata la TegetaEscrow
0 comments:
Post a Comment