| Kamanda wa polisi mkoa wa Pwani Ulrich Matei. |
Watu tisa wanadaiwa kuuawa katika mapigano baina ya
jamii ya wafugaji w kabila la Wabarbaig maarufu kama Wamang'ati na wasukuma
wilayani Kisarawe Mkoani Pwani.
Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa polisi
mkoa huo Ulrich Matei amesema chanzo cha mgogoro ni baada ya mfugaji jamii ya
Wamang'ati kutuhumiwa kuiba Ng'ombe zaidi ya watano wa mfugaji wa kisukuma.
Kamanda amesema baada ya wizi huo vijana wa Kisukuma
walianza msako na walimpomkamata mtuhumiwa walishambulia hadi kumuua na ndipo
wafugaji wa Kimang'ati walipoamua kulipiza kisasi.
Aidha Kamanda Matei amesema Uchunguzi zaidi unaendelea
ili kubaini majina ya watu waliouawa na kuwasaka watuhumiwa wa mauaji hayo.
0 comments:
Post a Comment