TETEMEKO LA ARDHI LAIPIGA CHINA

 

BEIJING — Tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa 6.3 limepiga katika eneo la jimbo la Sichuan kusini magharibi mwa China na kusababisha kifo cha mtu mmoja, shirika la habari la nchi hiyo Xinhua limeripoti.

Tetemeko hilo limepiga umbali wa kilometa 40 kutoka mji wa Kangding kwenye kina cha kilometa 18, kwa mujibu wa taarifa za Kituo cha Matetemeko cha nchi hiyo.

Majengo yanaripotiwa kutikisika sana na mwanamke mmoja kikongwe kufa baada ya kupigwa na kioo kilichovunjika.

Wakazi wa mji mkuu wa jimbo hilo, Chengdu, waliathiriwa na tetemeko hilo.


Matetemeko ya ardhi hulipa mara kwa mara eneo la kusini magharibi mwa China. Mwaka 2008 tetemeko la ardhi liliua watu wapatao 70,000 katika jimbo hilo la Sichuan.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment