SULLEY MUNTARI AONDOLEWA KATIKA KIKOSI CHA BLACK STARS
Chama cha Soka cha Ghana (GFA) kimemsimamisha mara moja Sulley Ali Muntari bila kikomo kushiriki katika kikosi cha timu ya taifa ya nchi hiyo, Black Stars.
Uamuzi huo umechukuliwa kutokana na kitendo cha Muntari kumshambulia kwa makusudi Mjumbe wa Kamati Tendaji ya Chama hicho na Mjumbe wa Menejimenti ya Black Stars, Bwana Moses Armah siku ya Jumanne tarehe 24 Juni, 2014 wakati wa kikao.
Ushiriki wa Muntari katika michuano ya Kombe la Dunia 2014 umesitishwa mara moja.
Chanzo: Ghanafa.org
0 comments:
Post a Comment