SOMA STORI YA CRISTIANO RONALDO AMEROGWA NA MGANGA WAKIENYEJI WA GHANA ILI ASICHEZE KOMBE LA DUNIA.

Mbwembwe na matukio ya kushangaza yanazidi kuonekana kati ya nchi zinazopeleka timu zao Brazil kwa ajili ya Kombe la Dunia.
Mganga wa kienyeji wa Ghana anaejulikana kwa jina la Nana Kwaku Bonsam amewatoa wasiwasi raia wan chi hiyo wanaomhofia Cristiano Ronaldo katika mchezo kati ya Ghana na Ureno utakaofanyika June 26.

 Mganga huyo aliyewahi kutabiri mwezi February kuwa Ronaldo angezikosa fainali za Kombe la Dunia ameweka wazi kuwa yeye ndiye anaemroga mchezaji huyo ambaye Jumatano hii alitangazwa kuwa majeruhi anaesumbuliwa na goti.

 Nana Kwaku ambaye maana ya jina lake ni ‘Shetani wa Jumatano’ amesisitiza kuwa hakuna dawa yoyote itakayoweza kumponya mchezaji huyo hadi kombe la dunia litakapokwisha.
 “Ninafahamu sababu ya majeraha ya Cristiano Ronaldo, ninamfanyia kazi. Niko serious kuhusu hilo. Wiki iliyopita, nilizunguka nikitafuta mbwa wane na niliwapata, watatumika kutengeneza mzimu maalum unaitwa ‘Kahwir Kapam.” Alisema Mganga huyo kwenye maelezo yake.

 Balaa! Taarifa hii itapokelewaje na wananchi wa Ghana? Je, watampa sapoti wakimuombea adui yao njaa ili asiwe kikwazo kwao? Vipi Wareno watachukua hatua gani au watazipuuzia habari za mganga huyo wa kienyeji?
Share on Google Plus

About www.habarika24.blogspots.com

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment