RAIS WA MISRI KUAPISHWA LEO

Egypt President-elect Abdel Fattah el-Sisi
Rais mteule wa Misri Abdulfattah al-Sisi



Mkuu wa zamani wa jeshi la Misri, Abdul Fattah al-Sisi anaapishwa leo Juni 8, kuwa rais mpya wa Misri.

Shirika la habari la serikali ya nchi hiyo, MENA, limesema kuwa al-Sisi ataapishwa katika viwanja vya Mahakama Kuu ya Katiba.

Kwa mujibu wa taarifa huyo, rais wa mpito Adly Mansour, Waziri Mkuu Ibrahim Mahlab na baraza lake, Mkuu wa chuo Kikuu cha al-Azhar, Papa wa Kanisa la Wakopti Tawadros II, wanasiasa na watu wengine mashuhuri watahudhuria sherehe hiyo.

Shughuli hiyo inafanyika wiki moja baada ya uchaguzi uliofanyika Mei 28 na ambao ulichukua siku tatu mfululizo.

Katika matokeo yaliyotangazwa Juni 3, al-Sisi alitangazwa rasmi kuwa mshindi wa kinyang’anyiro hicho kwa asilimia 96.91 ya kura.

Uchaguzi huo umefanyika takriban mwaka mmoja baada ya al-Sisi kuongoza mapinduzi dhidi ya rais aliyechaguliwa kidemokrasia, Muhammed Mursi, Julai 2013.

Chama cha Musri cha Udugu wa Kiislamu na makundi mengine yanayopigania demokrasia nchini humo yaligomea uchaguzi huo, hatua iliyosababisha kushuka kwa kiwango cha ushiriki wa wapiga kura.

Operesheni za jeshi dhidi ya wafuasi wa Mursi zilisababisha vifo vya watu zaidi ya 1,400 na maelfu kufungwa jela huku mamia ya wafuasi wake wakihukumiwa kifo.


Ushindi wa al-Sisi unairudisha Misri mikononi mwa kiongozi wa kijeshi miaka mitatu baada ya maandamano yalimng’oa Mubarak, ambaye alikuwa ofisa wa jeshi la anga na aliyeitawala nchi hiyo kwa takribani miongo mitatu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment