MATOKEO YA UCHAGUZI WA MISRI

Egypt’s President-elect Abdel Fattah el-Sisi
Rais mteule wa Misri, Abdulfattah al-Sisi



Tume ya uchaguzi nchini Misri imemtangaza rasmi mkuu wa zamani wa jeshi la nchi hiyo, Abdul Fattah al-Sisi, kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika hivi karibuni nchini humo.

Tume hiyo imetangaza kuwa al-Sisi ameshinda kwa asilimia 96.1 ya kura zote zilizopigwa.

Aidha, tume hiyo imesema kuwa waliojitokeza kupiga kura ni asilimia 47.5 ya watu milioni  53 wenye sifa za kupiga kura. Hata hivyo, baadhi ya vyama na mirengo ya upinzani imesema kuwa waliojitokeza kupiga kura hawazidi asilimia 11.

Katika kinyang’anyiro hicho al-Sisi alimshinda mpinzani wake pekee Hamdeen Sabahi ambaye ameukosoa uchaguzi huo akisema kuwa ulikosa viwango.

Katika taarifa yake ya Mei 28, kampeni ya Sabahi ilitangaza kuwaondosha mawakala wake wa uchaguzi kwa sababu walikuwa wakitekwa au kushambuliwa.

"Ndani ya saa 48 zilizopita tumekuwa tukilengwa kwa kudhalilishwa, kushambuliwa na kuvunjiwa heshima. Mawakala wetu wamekuwa wakizuiliwa kuingia kwenye vituo vya kupigia kura, wamekuwa wakishambuliwa na kukamatwa,” ilisema taarifa hiyo.


Uchaguzi ulihitimishwa Mei 28 na kulazimika kuongezwa siku za upigaji kura  kufuatia ushiriki mdogo wa wananchi.

Vuguvugu maarufu la Udugu wa Kiislamu na makundi mengine yanayopigania haki za kidemokrasia yaligomea uchaguzi huo, hatua iliyosababisha ushiriki mdogo wa wapiga kura kuliko ule uliomuweka madarakani Rais aliyeondolewa, Muhammad Mursi.


Ushind wa al-Sisi umeiweka Misri mikono mwa kiongozi wa kijeshi miaka mitatu baada ya maandamano makubwa yaliyomuondoa Husni Mubarak ambaye alikuwa askari wa anga aliyeiongoza nchi hiyo kwa miongo mitatu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment