Rais wa Nigeria, Goodluck Ebele Jonathan |
Rais wa Nigeria Goodluck Jonathan amewahakikishia
Wanigeria kuwa uchaguzi mkuu wa nchi hiyo utafanyika kama ulivyopangwa licha ya
changamoto za kiusalama zinazoikumba nchi hiyo.
Akizungumza jana katika kanisa moja mjini Abuja, Rais
Jonathan alisema kuwa serikali yake inaendelea na mikakati yake ya kimaendeleo
na kisiasa licha ya changamoto hizo na kwamba uchaguzi huo wa urais na ubunge
utafanyika katika mazingira mazuri ya kidemokrasia na uhuru.
Aidha, Rais Jonathan amesisitiza kuwa programu za
mageuzi zinazotekelezwa na serikali yake sio programu hewa bali zimeanza kutoa
matunda ya kujivunia katika sekta muhimu kama vile kilimo, miundombinu,
nishati, viwanda na makazi.
Rais Jonathan aliwataka wananchi kuomba na kusali ili
kufanikisha juhudi za kuwakomboa wasichana zaidi ya 200 wanaodaiwa kutekwa na
kundi la Boko Haram.
0 comments:
Post a Comment