HUYU NDIYE MAMBA ALIELETA BALAA NDANI YA HOTELI!!

Alisema kuwa mamba huyo alitoka nyuma ya pori lililopo karibu na hoteli hiyo ambapo hata yeye alipoamka hakumuona na alining’iniza miguu yake huku mamba huyo akiwa chini ya kitanda ambapo alitoka kwenda kupata kifungua kinywa kwenye mgahawa wa hoteli hiyo.
 Inaelezwa kuwa mamba huyo aligundulika na mfanyakazi aliyekuwa akifanya usafi katika chumba hicho na kupiga mayowe yaliyomshtua Mr Whittall ambapo alitoka mbia kwenda kushuhudia kulikoni na kumkuta mamba huyo akiwa chini ya kitanda chake kumbe alilala naye kwenye chumba hicho usiku mzima.
Mamba ni wataalam wa kujificha na ndiyo maana hunusirika kuuwawa na wanyama wengine hususani binadamu hata wakiwa nje ya maji,alisema Mr Whittall.
Na huweza kutulia sehemu moja kwa muda mrefu bila kugundulika na myama yoyote hivyo kumtambua inakuwa ni vigumu hiyo ni kutokana na maumbile yao yalivyo na hukimbilia ndani ya vichaka au kuingia kwenye nyumba kama hotelini hapo kufuata joto hasa katika kipindi cha mvua na baridi kali na alipenda kukaa chini ya kitanda hicho kwasababu kulikuwa na joto.
Mkurugenzi huyo alilazimika kuwaita wafanyakazi wengine ambao walisaidiana kumuondoa mamba huyo kutoka kwenye chini ya kitanda na kumtupa kwenye bwawa la hoteli hiyo.


Share on Google Plus

About www.habarika24.blogspots.com

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment