Rais wa Afghanistan, Hamid Karzai |
Afghanistan imetishia
kuvishambulia vikosi vya Pakistan iwapo hawataacha kurusha makombora kwenye
vijiji vya Afghanistan.
Waziri wa
Ulinzi wa Afghanistan, Jenerali Bismillah Khan Mohammadi amesema kuwa vikosi
vya nchi yake viko tayari kuchukua hatua dhidi ya askari wa Pakistan iwapo
askari hao hawatoacha mara moja kurusha makombora kwenye vijiji vya vya nchi
yake vinavyopakana na Pakistan.
Hata hivyo, Jenerali
Mohammadi, aliwaambia wabunge kuwa jeshi la nchi hiyo halitachukua hatua hiyo
bila kupata amri ya serikali ya kujibu mapigo.
Onyo hilo
limekuja katika wakati ambao mivutano baina ya mataifa hayo mawili umepanda
katika miezi ya hivi karibuni kuhusu mashambulizi ya mpakani.
Maafisa wa Afghanistan
wanasema kuwa kwa uchache watu sita wameuawa na wengine 40 kujeruhiwa kutokana
na makombora yanayorushwa kutoka upande wa Pakistan katika siku za hivi
karibuni.
Aidha, jana
serikali ya Afghanistan ilionya kuwa itajiondoa kwenye mazungumzo kuhusu ulinzi
yanayoendelea baina ya mataifa hayo mawili kutokana na kulituhumu jeshi la
Pakistan kuwa limekuwa likifanya mashambulizi hayo.
Maafisa wa
usalama kutoka upande wa Afghanistan wameshasema kuwa hawatashiriki katika
mkutano wa kikanda kuhusu usalama uliopangwa kufanyika Juni 4 mjini Islamabad,
Pakistan.
Mnamo Mei 27, zaidi
ya makombora 300 yalirushwa kutoka upande wa Pakistan na kutua katika maeneo
mbalimbali ndani ya Afghanistan.
Mapema mwezi Mei,
afisa usalama mmoja wa Pakistan alipoteza maisha kutokana na risasi zilizotoka
upande wa Afghanistan katika mkoa wa milimani wa Bajaur, jambo ambalo
limezidisha mivutano baina ya mataifa hayo.
0 comments:
Post a Comment