| Waasi wa M23 wakiwa msituni katika Jimbo la Kivu Kaskazini nchini Kongo |
WAZIRI wa Mashaurı ya Kıgenı wa Jamhurı ya Kıdemokrasıa
ya Kongo, Raymond Tshibanda, amesema
kuwa siku ya Jumatatu serikali ya nchi hiyo itasaini makubaliano ya amani na
waasi wa kundi la M23.
Mnamo Novemba 5, kundi la M23 lilisema litaweka silaha
chini na kufanya mazungumzo ya amani baada ya ngome zake kudhibitiwa na jeshi
la Kongo katika milima ya Tshanzu na Runyoni kwenye mpaka wa Uganda na Rwanda.
Kwa mujibu wa msemaji wa serikali ya Uganda, Ofwono
Opondo, utiaji saini utafanyika katika mji mkuu wa Uganda, Kampala.
Waasi wa M23 walijiondoa katika jeshi la Kongo mwezi
Aprili 2012 kupinga kile walichodai kuwa ni mwenendo mbaya ndani ya jeshi la
Taifa (FARDC). Walikuwa wamejumuishwa katika jeshi chini ya mkataba wa amani
uliosainiwa mwaka 2009.
Tangu mwezi Mei 2012, takriban watu milioni 3
wameyekimbia makazi yao katika eneo la mashariki mwa Kongo. Takriban watu
milioni 2.5 ni wakimbizi wa ndani, huku zaidi ya watu 460,000 wamekimbilia
katika nchi za Rwanda na Uganda.
Kongo imekuwa ikikabiliwa na matatizo matatizo kwa
miongo kadhaa, kama vile umaskini uliokithiri, miondombinu mibovu, na vita
katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo ambavyo viliibuka tangu mwaka 1998 na
kugharimu maisha ya zaidi ya watu milioni 5.5.
0 comments:
Post a Comment