KIMBUNGA CHASABABISHA MAAFA MAKUBWA NCHINI UFILIPINO

Photo shows aftermath of super Typhoon Haiyan in Tacloban, in Leyte island on November 9, 2013.
Picha ikionesha hali halisi baada ya Kimbunga Haiyan katika mji wa Tacloban, kwenye kisiwa cha Leyte Novemba 9, 2013.




Na Kabuga Kanyegeri

MAAFISA wa Shirika la Msalaba Mwekundu nchini Ufilipino wanasema kuwa kwa uchache watu wapatao 1,200 wamepoteza maishha baada ya kimbunga Haiyan kuyapiga vibaya maeneo mawili nchini humo na kusababisha gharika kubwa kuikumba nchi hiyo inayopatikana Kusini Mashariki mwa bara la Asia.

Katibu Mkuu wa shirika hilo nchini Ufilipino, Gwendolyn Pang, amesema kuwa idadi hiyo ya vifo ilitokana na ripoti za awali za wafanya kazi wa shirika hilo waliokuwa wakistoa huduma mbalimbali za kibinaadamu.

Aidha, duru zinasema kuwa idadi ya vifo inatarajiwa kuongezeka wakati vikosi vya usalama vitakapoyafikia maeneo ya ambali ambayo yameharibiwa vibaya sana na kimbunga hicho kinachokwenda kwa kasi.

Zaidi ya Wafilipino milioni moja wamelazimika kuyakimbia makazi yao na kukimbilia maeneo salama.

Haya yanatokea baada ya Kimbunga Haiyan, ambacho ni miongoni mwa vimbunga vikubwa mno kuwahi kutokea, kukipiga kisiwa cha mashariki cha Samar kabla ya kwenda katika visiwa vingine vitano.

Taarifa za vyombo vya habari zinasema kuwa miongoni mwa maeneo yaliyoathiriwa vibaya ni kisiwa cha Leyte kilichopo mashariki mwa nchi hiyo na pwani ya mji wa Tacloban, ambako majengo yamebomolewa na miti kung’olewa. Kimbunga hicho pia kilisababisha mmomonyoko wa udongo, mafuriko na kukata umeme na mawasiliano katika visiwa kadhaa.

Aidha, kimbunga hicho kinatarajiwa kusababisha mvua katikati mwa nchi ya Vietnam kesho Jumapili. Pia, kinatarajiwa kusonga mbele na kuyaathiri vibaya maeneo ya pwani ya kusini mwa China.

Kwa mujibu wa maafisa, zaidi ya watu milioni 12 wapo katika hatari ya kuathiriwa na kimbunga hicho kikali.

Wastani wa vimbunga 20 huipiga nchi ya Ufilipino kila mwaka. Mwezi Desemba mwaka 2011, Kimbunga Washi kilisababisha vifo vya watu 1,200, kuwahamisha watu 300,000 na kuyaharibu zaidi ya makazi 10,000.

Mwaka jana kimbunga Bopha kilipiga katika miji mitatu ya pwani kwenye kisiwa cha Mindanao, kikaua watu 1,100 na kusababisha uharibifu unaokadiriwa kufikia Dola za Kimarekani bilioni 1.04.

Mwezi Septemba, Kimbunga Usagi, kilichokuwa kikisafiri kwa kasi ya kilometa 240 kwa saa, kilipiga katika kisiwa cha Batanes kilichopo kaskazini mwa nchi hiyo kabla ya kusababisha hasara kubwa nchini China.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment