MWANAUME ALIYEJIFANYA MWANAMKE AKAMATWA



mwanzia


Mwishoni mwa juma hili kumekuwepo na sintofahamu mjini Nairobi, nchini Kenya, baada ya mwanaume mmoja mwenye umri wa miaka 26 kukamatwa. Kwa muda mrefu kijana huyo amekuwa akiwadanganya wanaume wenzake kwa kujifanya kuwa ni mwanamke.

Mwanaume huyo alitengeneza matiti ya bandia ambapo alichukua glovu mbili na kuzijaza maji kisha akazipakachika vizuri ndani ya sidiria. Alivaa kama mwanamke na kuonekana mwenye mvuto kwa kuwa alikuwa ameyatengeneza makalio yake katika namna iliyowavutia wanaume.

Kwa mujibu wa wenzake, mtu huyo amekuwa akifanya hivyo kwa muda sasa na hawakuwahi kumshuku hata kidogo. Alionekana kama mwanamke na muda wote alivaa vizuri na kuwa na muonekano maridadi.

Akizungumza na wanahabari, mshukiwa huyo alikiri kwamba alianza kuvaa kama mwanamke na kufanya ukahaba tangu mwaka jana.

Alidai kuwa alikuwa akiikimu familia yake kwa hoja kwamba alitafuta kazi kwa miaka mingi bila mafanikio, hivyo akaamua kujiingiza katika mchezo huo.

Alisema kuwa alifurahia uhusiano na wanaume wengi na kwamba anahuzunika kwa kubainika wakati alikuwa anahitaji kuendelea na shughuli yake.


CHANZO: kenyan-post
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment