Watu wenye silaha wameushambulia msafara wa harusi
katika, nchini Nigeria na kuua zaidi ya watu 30, kwa mujibu wa mashuhuda na
manusura.
Msemaji wa serikali ya jimbo la Amadawa, Ahmad Sajo amesema
kuwa sherehe ya harusi ilifanyika katika kijiji cha Fugi, ambapo bwana harusi
na wageni mbalimbali walikuwa wakielekea nyumbani ndipo waliposhambuliwa kwenye
barabara kuu kati ya miji ya Bama na Gwoza katika jimbo jirani la Maiduguri.
Barabara hiyo hupitia kwenye misitu inayojulikana kuwa maficho ya waasi na
makundi mbalimbali yenye silaha.
Mpaka sasa hakuna kundi lililodai kuhusika, ingawa
serikali inalitupia lawama kundi la Boko Haram, ambalo linadaiwa kujihusisha na
matukio kama hayo.
Wiki iliyopita, kundi hilo lilikishambulia kizuizi cha
jeshi kwenye barabara hiyo na mashuhuda wanasema kuwa kwa uchache askari 4 wa
serikali waliuawa.
Mashambulizi mbalimbali yamekuwa yakiendelea licha ya
jeshi kuwafukuza waasi hao katika miji mikubwa ya eneo la kaskazini mashariki
huku maeneo hayo yakiwa chini ya hali ya hatari iliyotangazwa miezi mitano
iliyopita.
0 comments:
Post a Comment