KIONGOZI WA M23 ATAKA KUSIMAMISHWA MAPIGANO


A group of M23 rebels walk through the jungle in North Kivu province. (file photo)
Waasi wa M23 wakitembea msituni katika jimbo la Kivu Kaskazini



Kiongozi wa kundi la waasi la M23 la nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Bertrand Bisimwa, ametaka kusimamishwa mapigano na vikosi vya serikali katika jaribio la kutaka kuendeleza mazungumzo ya amani na serikali ya Kongo.

Bisimwa amesema kuwa lengo lake ni “kuruhusu muendelezo wa mchakato wa kisiasa” na wasimamizi wa mazunguzo ya amani yanayoendelea nchini Uganda.

Hili limekuja baada ya Uganda kutoa wito wa kusimamishwa kwa mgogoro uliodumu kwa takriban miezi 20 baina ya jeshi la Kongo na waasi wa M23.

Tangu Jumatano, Kampala imekuwa mwenyeji wa awamu mpya ya mazungumzo ya amani, siku kumi baada kuvunjika kutokana na waasi wa M23 kuweka sharti la kusamehewa kwa viongozi wao wote.

Roger Lumbala, mwakilishi mkuu wa M23 kwenye mazungumzo hayo, alisema kuwa waasi walikuwa tayari kusaini mkataba wa amani iwapo wangepokea mwaliko kutoka kwa wasimamizi wa mazungumzo hayo.

Hata hivyo, jeshi la Kongo liliapa kuyafutilia mbali makundi yote ya waasi.

Makundi kadhaa yenye silaha, ikiwemo M23, wanaendesha harakati zao za uasi mashariki mwa Kongo na wanapigania kuidhibiti nchi hiyo kubwa yenye maliasili za madini, kama vile dhahabu, urani, coltan, ambayo hutumika katika utengenezaji wa vifaa vingi vya elektroniki, ikiwemo simu za mkononi.

Waasi wa M23 walijiondoa katika jeshi la Kongo mwezi Aprili 2012 kupinga kile walichodai kuwa ni mwenendo mbaya ndani ya jeshi la Taifa (FARDC). Walikuwa wamejumuishwa katika jeshi chini ya mkataba wa amani uliosainiwa mwaka 2009.

Tangu mwezi Mei 2012, takriban watu milioni 3 wameyekimbia makazi yao katika eneo la mashariki mwa Kongo. Takriban watu milioni 2.5 ni wakimbizi wa ndani, huku zaidi ya watu 460,000 wamekimbilia katika nchi za Rwanda na Uganda.


Kongo imekuwa ikikabiliwa na matatizo matatizo kwa miongo kadhaa, kama vile umaskini uliokithiri, miondombinu mibovu, na vita katika eneo la mashariki mwa nchi hiyo ambavyo viliibuka tangu mwaka 1998 na kugharimu maisha ya zaidi ya watu milioni 5.5.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment