MILIPUKO YAENDELEA KUITIKISA MALI


 The site of a car bomb explosion in Mali (file photo)


WATU Sita, wakiwemo raia wawili, wamepoteza maisha na wengine kadhaa kujeruhiwa katika mlipuko wa bomu uliotokea jirani na kambi moja ya jeshi kaskazini mwa Mali.

Tukio hilo lilitokea jana Jumamosi baada ya gari lililokuwa na mabomu kulipuka katika mji wa Timbuktu ulio kaskazini mwa nchi hiyo.

Ripoti zinasema kuwa askari sita wa jeshi la nchi hiyo ni miongoni mwa walioathiriwa na mlipuko huo, huku nyumba kadhaa zikiharibiwa kabisa.

Serikali ya Mali imelaani vikali shambulizi hilo, ambalo limetekelezwa siku kadhaa baada ya wapiganaji wa Tuareg wanaopigania kujitenga kwa eneo la kaskazini kusitisha mazungumzo na serikali, wakiituhumu kwa kushindwa kutekekeleza ahadi zake kuhusu makubaliano ya amani.

Mwezi Juni viongozi wa Kituareg na viongozi wa mpito wa serikali ya Mali walifikia makubaliano ya kuliruhusu jeshi kurudi katika eneo la Kidal na kufanyika kwa uchaguzi wa urais.

Tukio la jana ni la pili kufanywa dhidi ya vikosi vya jeshi tangu Septemba 26.

Rais wa Mali, Ibrahim Boubacar Keita, amelifanya suala la maridhiano kuwa kipaumbele chake cha juu cha utawala wake tangu aliposhinda uchaguzi wa urais uliofanyika Agosti mwaka huu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment