ASKARI 3 WA KENYA WALIUAWA KATIKA SHAMBULIZI LA WESTGATE





ASKARI watatu wa Kenya walipoteza maisha yao wakati wakipambana kuwaokoa mateka katika shambulizi kwenye Jumba la Kibiashara la Westgate mjini Nairobi.

Askari wengine 8 wapigania maisha yao hospitalini baada ya kujeruhiwa kwenye operesheni hiyo.

Mkuu wa Vikosi vya Ulinzi vya Kenya (KDF), Jenerali Julius Karangi alisema kuwa askari 11 walijeruhiwa na kupelekwa kwenye hospitali ya jeshi kwa matibabu. “Kwa bahati mbaya watatu kati yao walipoteza maisha.”

Taarifa iliyotolewa na msemaji wa jeshi, Kanali Cyrus Oguna inasema kuwa KDF walionesha ari kubwa katika juhudi za kutekeleza operesheni ndani ya jengo la Westgate.

“Mazingira tata na hatari ya tukio hili yalihitaji uangalifu na tahadhari ya hali ya juu kuhakikisha usalama wa mateka. KDF ilifanya kazi hii kwa kiwango cha hali ya juu kabisa cha weledi.” Alisema Oguna katika taarifa hiyo.

Mkuu wa vikosi vya ulinzi, Jenerali Karangi alizifariji familia za askari waliouawa na kuwaelezea kuwa mashujaa walioitoa damu yao kwa ajili ya ulinzi wa taifa.

“Tunapenda kuwathibitishia kuwa matukio kama hayo hayarudisha nyuma ari ya KDF ya kuhakikisha kwamba amani na uthabiti vinapatikana nchini Somalia na katika ukanda huu.” Iliongeza taarifa hiyo.


CHANZO: KTN KENYA
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment