ISRAELI YAIDONDOSHA 'DRONE' YA HIZBULLAH

A file photo shows Israeli F-16 fighter jets.
Ndege za kivita za Israeli aina ya F-16



Jeshi la Israeli limesema kuwa limetungua ndege isyokuwa na rubani (drone) inayomilikiwa na Hezbollah karibu na bandari ya kaskazini ya Haifa.


Shirika la habari la AP limemnukuu msemaji wa jeshi akisema kuwa ndege hiyo ilitambuliwa ikiwa katika anga ya Lebanon kilometa nane kutoka pwani ya magharibi mwa Haifa na kudondoshwa na ndege ya jeshi la Israeli aina ya F-16.


Ndege iliyokuwa imembeba Waziri Mkuu wa Israeli, Benjamin Netanyahu, ambaye alikuwa akifanya ziara katika eneo la kaskazini la nchi hiyo, ililazimishwa kutua kufuatia hatua ya 'drone' hiyo kuingia katika anga la Israeli.


Katika taarifa yake, Netanyahu alisema kuwa tukio hilo ni “zito mno.” 

Inaelezwa kuwa meli za Israeli zinatafuta mahali ndege hiyo ilipodondokea.

Aidha, mwezi Oktoba, mwaka jana, ndege kama hiyo iliyotumwa na Hezbollah ilipenya ndani kabisa ya Israel kabla ya kuangushwa na makombora ya Israeli. 
Share on Google Plus

About mahamoud

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment