185 wauawa katika mapigano nchini Nigeria

185 wauawa katika mapigano nchini Nigeria




Watu wasiopungua 185 wameuliwa kaskazini mashariki mwa Nigeria katika mapigano kati ya vikosi vya jeshi la nchi hiyo na wapiganaji wa Boko Haram. Lewa Kole afisa wa serikali za mitaa amemueleza gavana wa jimbo la Borno Kashin Shettima kuwa mapigano yalianza Ijumaa iliyopita huko Baga katika jimbo la Borno na kudumu kwa masaa kadhaa.

Hata hivyo bado haijafahamika ni askari, raia au wanamgambo wangapi wa Boko Haram waliouliwa katika mapigano hayo kwa kuzingatia kuchomwa moto viwiliwili vingi ambavyo havijaweza kutambuliwa, kufuatia moto ulioteketeza karibu mji huo wote. Brigedia Jenerali Austin Edokpaye amesema kuwa raia wengi walitumiwa na wapiganaji wa Boko Haram kama ngao ya binadamu katika mapigano hayo.

Share on Google Plus

About mahamoud

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment