SOMALIA YAPATA WAZIRI MKUU MPYA

Somalia
Waziri mkuu mpya wa Somalia  Omar Abdirashid Ali Sharmarke akizungumza kufuatia uteuzi wake mjini  Mogadishu, Somalia, Desemba 17, 2014.



Rais wa Somalia Hassan Sheikh Mohamud amemteau balozi wa nchi hiyo nchini Marekani kuwa waziri mkuu kufuatia kuondolewa kwa aliyekuwa waziri mkuu mapema mwezi huu.

Akiwa katika viwanja vya Ikulu mjini Mogadishu leo mchana, Rais Mohamud alimteua mwanasiasa mzito mwenye umri wa miaka 54, Omar Abdirashid Ali Sharmarke kuchukua wadhifa huo.

"Nina furaha kumteua Omar Abdirashid Ali kuwa waziri mkuu mpya wa nchi yetu. Ninatarajia kuwa atatekeleza majukumu yake,” alisema rais huyo.

Rais Mohamud aliongeza kuwa Somalia iko njia panda na inahitaji waziri mkuu mpya atakayeweka mipango makini kwa ajili ya mustakbali wa kisiasa wa nchi hiyo.

Kwa upande wake Sharmarke alisema kuwa ataendeleza juhudi za kuleta uthabiti na kuipeleka nchi kwenye uchaguzi ulio huru.

Sharmarke anachukua nafasi ya Abdiweli Sheikh Ahmed Mohamed, ambaye bunge lilipiga kura kumuondoa siku 11 zilizopita kutokana na mzozo mkubwa uliokuwepo kati yake na Rais wa nchi hiyo kuhusu mabadiliko ya baraza la mawaziri na kuondolewa kwa mkuu wa upelelezi wa nchi hiyo.


Umoja wa Mataifa, Marekani na Muungano wa Ulaya zilionesha wasiwasi kuhusu mgogoro uliokuwa ukiendelea katika Ikulu ya Somalia.

Sharmarke aliwahi kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo katika serikali ya mpito iliyokuwa ikiungwa mkono na jumuiya ya kimataifa kati ya mwaka 2009 na 2010. Alijiuzulu baada ya kushindwa kuelewana na Rais wa wakati huo Sheikh Sharif Sheikh Ahmed.

Sharmarke anakabiliwa na changamoto kubwa za kupambana na ufisadi, kulishinda kundi la al-Shabab na kuijenga upya Somalia iliyoharibiwa na vita.


Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Nicholas Kay amesema kuwa nchi hiyo ina mlima mkubwa wa kupanda ili kupitia katiba na kufanya kura ya maoni itakayofuatiwa na uchaguzi mwaka 2016.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment