KENYA YAFUTA MASHIRIKA ZAIDI YA 500, BAADHI YATUHUMIWA KUFADHILI UGAIDI


Deputy director of Kenya’s NGO Coordination Board, Henry Ochido (L), sits in on a briefing in Nairobi on December 16, 2014, that 15 NGOs had been deregistered for allegedly financing terrorism activities.
Naibu Mkurugenzi wa Bodi ya Uratibu wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali nchini Kenya,  Henry Ochido (kushoto), akiwa katika mkutano na waandishi wa habari mjini  Nairobi Desemba 16, 2014, ambapo alieleza kuwa mashirika 15 yamefutiwa usajili kwa tuhuma za kufadhili shghuli za kigaidi.


Serikali nchini Kenya imeyafunga zaidi ya mashirika (NGOs) 500, baadhi yake yakituhumiwa kufadhili ugaidi.

Naibu mkurugenzi wa Bodi ya Kuratibu mashirika yasiyokuwa ya kiserikali, Henry Ochido, amesema kuwa jumla ya mashirika 15 kati ya 537 hayo, akunti zake zimefungwa na taarifa zake kupelekwa kwenye idara za usalama kwa kuhusishwa na ugaidi.

“Baadhi ya mashirika yamekuwa na yameendelea kutumika katika vitendo vya uhalifu, ikiwa ni pamoja na kufadhili ugaidi nchini Kenya na katika eneo la Pembe ya Afrika,” ilisema taarifa ya bodi hiyo.

Orodha hiyo inajumuisha mashirika 510 – yakiwemo makundi ya uwezeshaji kwa wanawake, mashirika ya maendeleo vijijini na makundi ya kusaidia watu wanaioshi na virusi vya Ukimwi- ambayo yamedaiwa kukiuka sheria ya masharika yasiyokuwa ya kiserikali nchini humo na kushindwa kujibu taarifa ya kusudio la kufutwa kwa vyeti vya usajili wao.

Mashirika mengine 12, ikiwa ni pamoja na shirika la Madaktari wasiokuwa na Mipaka (Medecins Sans Frontieres) na Concern Worldwide, yanatarajiwa kufutiwa usajili kwa sababu ya kushindwa kuwasilisha ripoti za mahesabu yake.

Mamia ya mashirika yasiyokuwa ya kiserikali yapo hatarini kufutiwa usajili ndani ya kipindi cha wiki tatu zijazo, amesema Ochido.

Wataalamu wameikosoa sheria ya mashirika yasiyokuwa ya kiserikali ya mwaka 1990 kuwa ni yenye kasoro nyingi, ambapo huifanya serikali kuyaingilia mashirika hayo na kuyanyima uhuru wa kujiendesha.


Kwa sasa Kenya ina zaidi ya askari 3,000 kusini mwa Somalia, ambapo wamekuwa wakipambana na wapiganaji wa al-Shabab. Uamuzi huo ulichukuliwa mwaka 2011, baada ya kundi hilo kudaiwa kufanya mashambulizi kadhaa ndani ya Kenya.


Kundi hilo limekuwa likidai kuhusika na mashambulizi mbalimbali nchini Kenya, likisema kuwa linalipiza kisasi dhidi ya uwepo wa maelfu ya askari wa Kenya nchi Somalia ambao ni sehemu ya kikosi cha Umoja wa Afrika kinachoisaidia serikali ya Mogadishu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment