UTEGUAJI WA BOMU LILILOACHWA KATIKA VITA YA PILI YA DUNIA WAHAMISHA WATU 20,000

Evacuated people wait in the Westfalen Halle hall in Dortmund, Germany, Sunday Nov. 3, 2013. (AP Photo/dpa,Marcus Simaitis)
Watu waliohamishwa kwenye makazi yao wakisubiri katika ukumbi wa Westfalen Halle mjini Dortmund, Ujerumani leo Jumapili Nov. 3, 2013.





ZAIDI ya watu 20,000 wameondolewa katika makazi yao katika mji wa Dortmund, magharibi mwa Ujerumani, wakati mamlaka zikijiandaa kutegua bomu kubwa lililoachwa wakati wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia.

Bomu hilo lenye uzito wa kilogramu 1,800 liligunduliwa baada ya wataalamu kuzichambua picha mbalimbali zilizopigwa na ndege maalumu iliyokuwa ikitafuta silaha zilizodondoshwa na majeshi ya Washirika kwenye eneo la viwanda la mkoa wa Ruhr nchini Ujerumani.

Bomu kama hilo lililopatikana miaka miwili iliyopita lilipelekea kuhamishwa kwa  watu wapatao 45,000 katika mji wa Koblenz karibu na mto Rhine.  


CHANZO: Global News
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 comments:

Post a Comment