Watu 15 wakiwemo watoto 13 wamekufa maji katika Ziwa
Tanganyika, baada ya mtumbwi mkubwa waliokuwa wakisafiria kutoka kwenye kijiji
cha Kipwa katika wilaya ya Kalambo Mkoani Rukwa , kuelekea katika kijiji cha
Kapele kufuata huduma za kliniki
kupinduka ndani ya ziwa hilo.
Mganga mkuu wa Wilaya ya Kalambo Dakta Hosea Mang'ombe,
amesema kufuatia kijiji cha Kipwa kilichoko kwenye mwambao wa ziwa Tanganyika
kukosa huduma ya zahanati, wananchi wa kijiji hicho wamejiwekea utaratibu wa
kupata huduma hiyo kwenye kijiji cha Kapele kilichoko umbali wa zaidi ya
kilonita 10, na ndipo walipokumbwa na balaa hilo ambapo pia wanahisi kuwepo kwa
mama mjamzito ambaye hadi sasa hajaonekana .
akithibitisha kuhusu tukio hilo kamanda wa polisi wa
mkoa wa Rukwa Bw Jacob Mwaruanda, amesema jeshi hilo linaendelea kuchunguza juu
ya ajali hiyo mbaya, na kutafuta miili ya baadhi ya watu ambao walikuwa
hawajapatikana bado hadi sasa.
CHANZO: ITV
0 comments:
Post a Comment